Rais Barack Obama na
Mkewe Michelle wamekuwa na wakati mzuri nchini Argentina ambapo
wameonekana wakisakata muziki wa aina ya Tango Jijini Buenos Aires
wakati wa hafla ya mlo wa usiku walioandaliwa na mwenyeji wao.
Rais Obama yupo Buenos
Aires kukutana na kiongozi wa Argentina Mauricio Marcri baada ya
kumaliza ziara yake ya Cuba, na amekuwa akipuuzia wito wa kumtaka
kurejea Marekani kufuatia mashambulizi ya Jijini Brussels, Ubelgiji.
Rais Obama ambaye
amesema hakubali magaidi waharibu ratiba yake alionekana jana usiku
akicheza katika mlo alioandaliwa na Ikulu ya Argentina akiwa na mkewe
Michelle pamoja na mke wa rais wa Argentina Juliana Awada.
Rais Obama akionyesha kuimudu miondoko ya Tango
Naam mambo ya Tango hayo rais Obama akienda nayo sambamba
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni