Sungura tisa wamekutwa wakiwa hai
kwenye kifusi cha jengo lililoanguka eneo la Huruma Jijini Nairobi
nchini Kenya na kuibua matumaini ya kupata watu wakiwa hai.
Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya
jana iliposti kwenye twitta yake kuhusu wanyama hao waliokutwa wakiwa
wamekwama kwenye jengo hilo la ghorofa baada ya siku tano kupita.
Tukio hilo limekuja ikiwa siku moja
tu, tangu mtoto wa miezi saba kuibuliwa akiwa hai kwenye vifusi
kutoka kwenye jengo hilo baada ya siku nne kupita.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni