.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 20 Juni 2016

ALBANIA YAPATA USHINDI WAKE WA KWANZA WA KIMATAIFA


Timu ya taifa la Albania imepata ushindi wake wa kwanza katika michuano ya kimataifa huko Lyon dhidi ya Romania na kupata matumaini ya uwezekano wa kutinga hatua ya 16 bora ya michuano ya Euro 2016.

Timu hiyo inayonolewa na Giovanni de Biasi imemaliza katika nafasi ya tatu  kundi A, na sasa watabidi kungojea iwapo wataibuka namba tatu bora kati ya timu nne zinazoshiriki michuano hiyo.

Katika mchezo huo mchezaji wa FC Zurich, Armando Sadiku, aliifungia Abania goli pekee katika mchezo huo, baada ya kupiga mpira wa kichwa uliomshinda golikipa wa Romania Ciprian Tatarusanu na kujaa wavuni.
                  Armando Sadiku akiifungia Albania goli pekee katika mchezo huo
                         Ermir Lenjani akikosa goli la wazi baada ya kupaisha mpira juu


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni