.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 20 Juni 2016

WATU SITA WAUWAWA KASKAZINI MWA MEXICO KATIKA MAPAMBANO

Watu sita wameuwawa kaskazini mwa Mexico katika mapambano baina walimu waliokuwa wakiandamana na polisi.

Katika mapambano hayo watu wengine 50, wakiwemo maafisa polisi wamejeruhiwa.

Tukio hilo limetokea katika jimbo la Oaxaca, ambako viongozi wa juu wawili wa chama cha walimu walikamatwa wiki iliyopita kwa tuhuma za rushwa.

Wanachama wa chama hicho cha walimu cha CNTE, ambacho kinahistoria ya uanaharakati makali, wamefunga barabara kusini mwa Mexico tangu viongozi wao wakamatwe.
              Athari za ghasi za maandamano hayo ya walimu katika jimbo la Oaxaca
Basi likiwa linateketea kwa moto kufuatia ghasi za maandamano hayo ya walimu kupinga viongozi wao kukamatwa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni