Timu ya Kikapu ya Cleveland
Cavaliers imebadilisha muelekeo wa fainali za NBA baada ya kupata
ushindi wa pointi 115-101 alfajiri ya leo dhidi ya Golden State
Warriors na kulazimisha kuwapo mchezo wa saba wa fainali.
Nyota LeBron James aliiongoza
Cavaliers, kupata ushindi huo baada ya kuwa nyuma kwa ushindi mara
3-1 wa michezo ya fainali na sasa itachezwa fainali ya saba jumapili
huko Oakland ili kuamua nani bingwa wa NBA Marekani.
LeBron James akidanki na kufunga kikapu
Stephen Curry akijaribu kumdhibiti LeBron James



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni