.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 21 Julai 2016

KOCHA PEP GUARDIOLA AKARIBISHWA NA KIPIGO BAYERN MUNICH

Kocha Pep Guardiola amekaribishwa kwa kipigo wakati aliporejea katika dimba la Allianz Arena, katika mchezo wake wa kwanza kama kocha wa Manchester City dhidi ya timu yake ya zamani ya Bayern Munichi.

Katika mchezo huo uliopigwa jana Guardiola aliyeonekana mchangamfu mno baada ya kukaribishwa vyema na klabu yake hiyo ya zamani, na mara kwa mara alionekana akitoa maelezo kwa wachezaji aliokuwa anawabadilisha.

Goli pekee katika mchezo huo lilifungwa na Erdal Ozturk katika dakika 14 kabla ya kumalizika kwa mchezo huo, kwa shuti lililougonga mguu wa Gael Clichy na kumpoteza mahesabu kipa wa Manchester City.
           Mchezaji Erdal Ozturk akiachia shuti lililozaa goli pekee la Bayern Munich
           Pep Guardiola akitoa maelezo kwa Yaya Toure kabla ya kumuingiza dimbani
   Mshambuliaji wa Bayern Munich Frank Ribery akiangalia jezi yake iliyochanika

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni