.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 21 Julai 2016

SAM ALLARDYCE KUTANGAZWA KUWA KOCHA MKUU WA UINGEREZA

Kocha Sam Allardyce anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Uingereza, huku uthibitisho rasmi ukitarajiwa kubainika hii leo.

Kocha Allardyce ataachana na klabu ya Sunderland baada ya miezi tisa katika klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza.

Allardyce, 61, anachukua nafasi ya kocha Roy Hodgson, ambaye alijiuzulu mwezi Juni baada ya kushindwa na timu ya Iceland katika hatua ya 16 bora ya miuchuano ya Euro 2016.

Allardyce, ambaye aliwahi kuzinoa West Ham, Newcastle na Bolton, aliongea na Chama cha Soka cha Uingereza, (FA) wiki iliyopita na amempiku kocha wa Hull, Steve Bruce.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni