.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 23 Julai 2016

MAJERUHI USAIN BOLT ASHINDA MBIO ZA MITA 200

Usain Bolt ameonyesha kuboreka afya yake kabla ya michuano ya Olimpiki mwezi ujao, baada ya kushinda mbio za mita 200 katika uwanja wa Olimpiki wa London.

Bingwa huyo wa Olimpiki mara sita alitumia muda wa sekunde 19.89, akiwa mbele ya mwanariadha wa Panama Alonso Edward aliyeshika nafasi ya pili.

Muingereza bingwa wa medali ya fedha ya Jumuiya ya Madola Adam Gemili alishika nafasi ya tatu akitumia muda wa sekunde 20.07.

Uwezo wa Bolt kufanya vyema ulikuwa ukitiliwa shaka baada ya kutoweza kushiriki majaribio ya kufuzu kushiriki michuano ya Olimpiki, kutokana na jeraha.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni