.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 26 Agosti 2016

BAHILI ARSENE WENGER AJITUTUMUA NA KUTOA PAUNDI MILIONI 50 KWA USAJILI

Kocha mgumu wa kutoa fedha za kununua wachezaji Arsene Wenger ametumbukiza mkono mfukoni na kutoa kitita cha paundi milioni 50 kuwanasa wachezaji beki Shkodran Mustafi na mshambuliaji Lucas Perez, kabla ya muda wa usajili haujaisha.

Ombi la Arsenal ambayo imeanza kwa kusuasua katika msimu huu wa Ligi Kuu ya Uingereza limekubaliwa na wachezaji hao wawili, na sasa inaamini kuwa itafanikisha kukamilisha mpango huo kabla ya kufungwa kwa usajili jumatano.

Iwapo mpango huo utakamilika unatarajiwa kupunguza shinikizo kwa Wenger ambaye mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakishikiza kuboreshwa kwa kikosi baada ya kuambulia pointi moja tu katika michezo yao miwili ya Ligi Kuu.
                Beki wa kati wa Valencia Shkodran Mustafi ambaye Arsenal wanamuwania
         Mshambuliaji wa Deportivo La Coruna Lucas Perez kulia anawaniwa na Arsenal 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni