.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 21 Agosti 2016

CHELSEA MWENDO MDUNDO, ARSENAL NA LEICESTER NGUVU SAWA

Mshambuliaji Diego Costa ameifungia goli la ushindi Chelesa kwa mara ya pili katika michezo miwili mfululizo baada ya kutoka nyuma kwa goli moja hadi kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Watford.

Watford walikuwa wa kwanza kupata goli kupitia kwa Eyienne Capoue na kuifanya kuongoza katika dakika ya 56, wakati wenyeji hao wakionekana kuumiliki mchezo huo katika dimba la Vacarage Road.

Hata hivyo mchezaji aliyetokea benchi Michy Batshuayi alisawazisha goli la kwanza kwa Chelsea tangu ahamie klabu hiyo, na kisha baadaye Diego Costa aliikimbilia pasi ya Cesc Fabregas na kumfunga kwa tobo kipa Heurelho Gomes.
                   Michy Batshuayi akishangilia goli lake la kwanza akiwa na Chelsea 
                                                   Diego Costa akiifungia Chelsea goli la ushindi
Wakati huo huo Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza Leicester City na walioshika nafasi ya pili Arsenal wameshindwa tena kupata ushindi wao wa kwanza katika msimu huu baada ya kutoka sare tasa katika dimba la King Power.

Timu zote mbili zilikuwa zinalenga zilikuwa zinalengo la kuibuka na ushindi baada ya kupoteza michezo yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa Hull City na Liverpool lakini zilishindwa kutikisa nyavu.
                           Kipa Cech akijiandaa kudaka mpira uliopigwa na Jamie Vardy

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni