.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 30 Agosti 2016

KIONGOZI WA DUBAI AKUTA VITI VITUPU MAOFISINI BAADA YA KUFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA SIKU YA KAZI

Kiongozi wa Dubai Sheikh Mohammed bin Rashid amepatwa na mshangao baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za umma na kukutana na viti vitupu katika siku ya kazi huku maafisa waandamizi wa serikali wakiwa hawapo ofisini.

Sheikh Mohammed bin Rashid, alishangazwa na hali hiyo pale alipofanya ziara hiyo ya kushtukiza katika siku ya jumapili, alipokuwa akifanya ukaguzi siku hiyo ambayo ni siku ya kazi nchini Dubai.

Kufuatia hali hiyo ya uzembe mkubwa wa watumishi wa umma maafisa tisa waandamizi wa Manispaa ya Dubai wameagizwa kustaafu, baada ya ziara hiyo ya kushtukiza ya Sheikh Mohammed bin Rashid.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni