Kiongozi wa Dubai Sheikh Mohammed
bin Rashid amepatwa na mshangao baada ya kufanya ziara ya kushtukiza
katika ofisi za umma na kukutana na viti vitupu katika siku ya kazi
huku maafisa waandamizi wa serikali wakiwa hawapo ofisini.
Sheikh Mohammed bin Rashid,
alishangazwa na hali hiyo pale alipofanya ziara hiyo ya kushtukiza
katika siku ya jumapili, alipokuwa akifanya ukaguzi siku hiyo ambayo
ni siku ya kazi nchini Dubai.
Kufuatia hali hiyo ya uzembe mkubwa
wa watumishi wa umma maafisa tisa waandamizi wa Manispaa ya Dubai
wameagizwa kustaafu, baada ya ziara hiyo ya kushtukiza ya Sheikh
Mohammed bin Rashid.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni