.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 27 Agosti 2016

LIGI KUU YA UINGEREZA CHELSEA MWENDO MDUNDO, LIVERPOOL YABANWA

Eden Hazard ambaye ameanza msimu huu akiwa kwenye kiwango kizuri ameifungia Chelsea goli moja katika ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Burnley.

Katika mchezo huo Hazard alikuwa wa kwanza kufunga goli kwa shuti la kuzungusha, kabla ya Willian kuongeza la pili, na kisha Victor Moses kufunga goli la tatu.
                              Eden Hazard akiachia shuti la kuzungusha lililojaa wavuni
                                                Victor Moses akifunga goli la tatu la Chelsea
Katika mchezo mwingine Liverpool imejikuta ikilazimwishwa sare ya goli moja kwa moja na Tottenham Hotspur, katika dimba la White Hart Lane.

Liverpool ilipata goli lake la kwanza kwa mkwaju wa penati uliopigwa na Milner baada ya Erik Lamela kumfanyia madhambi Roberto Firmino.

Tottenham walipambana kiume wasiaibishwe nyumbani na alikuwa Danny Rose aliyesawazisha goli katika kipindi cha pili
              Milner akijipinda na kuachia shuti la mkwaju wa penati na kuifungia Liverpool goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni