.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 27 Agosti 2016

MABINGWA WATETEZI LEICESTER CITY YAZINDUKA NA KUPATA USHINDI WA KWANZA NYUMBANI

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza timu ya Leicester City wamepata ushindi wao wa kwanza wakiwa nyumbani baada ya kuifunga Swansea magoli 2-1.

Leicester City walikuwa wa kwanza kupata goli kupitia kwa Jamie Vardy kisha baadaye Wes Morgan akaifungia goli la pili.

Riyad Mahrez alikosa penati baada ya Shinji Okazaki kufanyiwa rafu. Katika kipindi cha pili Swansea ilicharuka na alikuwa Leroy Fer aliyeifungia goli pekee mpira wa kichwa. 
               Jamie Vardy akiachia shuti lililoandika goli la kwanza la Leicester City
            Leroy Fer akiruka juu na kupiga mpira wa kichwa uliozaa goli pekee la Swansea

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni