Mabingwa
watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza Leicester City wameianza ligi hiyo kwa kuduwaza na kipigo cha magoli 2-1 kutoka kwa timu iliyopanda
daraja ya Hull City.
Kikosi
cha kocha Mike Phelam kiliongoza kwa kufunga goli lililofungwa kwa
pamoja na wachezaji Adama Diomande na Abel Hernandez hata hivyo goli
hilo alipewa Diomande.
Goli
hilo lilizawazishwa baadaye na Riyad Mahrez kwa njia ya penati baada
ya mchezaji mpya wa Leicester City Ahmed Musa kufanyiwa madhambi.
Hull
City ilipata goli la pili na la ushindi kupitia kwa Robert Snodgrass
baada ya krosi aliyoipiga kushindwa kuzuiliwa na mabeki.
Goli la Hull City lililofungwa na wachezaji wawili Adama Diomande na Abel Hernandez
Riyad Mahrez akipongezwa na wenzake baada ya kufunga goli kwa mkwaju wa penati
Robert Snodgrass akishangilia goli la pili na la ushindi kwa Hull City alilofunga




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni