.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 23 Agosti 2016

MADAKTARI WAMFANYIA UPASUAJI NYOKA ANACONDA NA KUMTOA UVIMBE

Madaktari wa wanyama nchini Thailand wamemfanyia upasuaji nyoka mkubwa aina ya anaconda mwenye umri wa miaka 10 na kufanikiwa kuondoa uvimbe uliokuwa karibu na moyo wake.

Nyoka huyo alipewa dawa za usingizi katika upasuaji huo uliofanyika kwa muda wa saa saba, Dk. Taweesak Anansiriwattana wa hospitali ya wanyama ya Klongluang ameliambia shirika la habari la BBC.

Madaktari hao waliupasua mwili wa nyoka huyo na kuutoa uvimbe wa kilo 1, na kisha kuchukua sambuli zake kwa ajili ya vipimo vya kimaabara ili kubaini iwapo nyoka huyo alikuwa na saratani.
                      Nyoka anaconda akiwa amewekewa mirija ya oxygen mdomoni 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni