.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 23 Agosti 2016

WATU 1,900 WAMEUAWA NDANI YA WIKI SABA KATIKA MSAKO WA WAUZA 'UNGA' PHILIPPINE

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Philippine amesema zaidi ya watu 1,900 wameuwawa wakati wa msako dhidi ya biashara za dawa za kulevya katika muda wa wiki saba zilizopita.

Mkuu huyo Ronald dela Rosa ametoa maelezo hayo mbele ya baraza la seneti kuhusiana na ongezeko kubwa la mauaji tangu rais Rodrigo Duterte awe rais wa nchi hiyo.

Amesema kuwa operesheni za polisi zimeuwa watu 750, lakini vifo vingine bado vinafayiwa uchunguzi.

Rais Duterte alishinda urais akiwa na sera zake za msimamo mkali za kutokomeza biashara ya dawa za kulevya.
                                                                           Rais wa Philippine Rodrigo Duterte

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni