.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 28 Agosti 2016

MANCHESTER CITY YAENDELEZA UBABE, MIDDLESBROUGH YATOKA SARE

Timu ya Manchester City imeendeleza wimbi la ushindi na kuongoza Ligi Kuu ya Uingereza kwa tofauti ya idadi ya magoli baada ya kuifunga West Ham kwa magoli 3-1.

Katika mchezo huo Manchester City walikuwa wa kwanza kufunga goli kupitia kwa Raheem Starling na kisha baadaye Fernandinho aliongeza la pili kwa mpira wa kichwa.

Michail Antonio alipunguza tofauti ya magoli baada ya kuifungia West Ham katika kipindi cha pili, kabla ya Sterling kufunga la tatu katika dakika ya 90.
Fernandinho akiruka juu na kupiga mpira wa kichwa uliozaa goli la pili la Manchester City.
Timu ya Middlesbrough imeendeleza rekodi yao ya kutofungwa katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kutoka sare tasa na timu ya West Brom hii leo.

Katika mchezo huo beki wa kushoto Brendan Galloway alipata nafasi nzuri ya kufunga katika kipindi cha kwanza baada ya kupanda mbele lakini kipa wa Middlesbrough Brad Guzan alikuwa imara.
                          Kipa Brad Guzan akizuia mpira uliopigwa na James McClean 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni