.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 28 Agosti 2016

WEST HAM YANAMNASA MSHAMBULIAJI SIMONE ZAZA

Timu ya West Ham ya Uingereza imeinasa saini ya mshambuliaji wa Italia Simone Zaza akitokea Juventus kwa mkopo wa msimu mzima wa kiasi cha paundi milioni 4.3.

Makubaliano hayo ya kumtwaa Zaza yanaweza kuwa ya kudumu na kufikia ada ya paundi milioni 17, na nyongeza ya milioni 2.5 kulingana na atakavyokuwa anashuka dimbani.

Usajili huo ni wa 11 kwa West Ham katika majira ya joto, na umefikisha kiasi cha paundi milioni 60 zilizotumika kwa usajili.

Zaza, 25, alijunga na Juventus Julai 2015 na alifunga magoli nane katika michezo 24 aliyocheza.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni