.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 14 Agosti 2016

MO FARAH ASHINDA MBIO ZA MITA 10,000 NA KUWEKA REKODI UINGEREZA

Mwanariadha wa Uingereza Mo Farah mwenye asili ya Somalia amefanikiwa kutetea ubingwa wa mbio za mita 10,000 katika michuano ya Olimpiki na kutwaa medali ya dhahabu.

Katika mbio hizo Farah alijikuta akianguka katika raundi ya 10 baada ya kukwatuliwa kwa bahati mbaya na mwanariadha mwenzake Galen Rupp, lakini alinyanyuka na kuendelea.

Mwanariadha wa Kenya Paul Tanui alipambana vilivyo na kumpita Farah, lakini bingwa huyo alizidisha kasi na kumpita. Farah anakuwa Muingereza wa kwanza kushinda medali tatu za dhahabu za Olimpiki.
   Mo Farah akishangilia ushindi baada ya kufanikiwa kuibuka mbabe wa mbio za mita 10,000
                Mo Farah akiwa amepiga magoti na kumshukuru Mungu kwa ushindi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni