.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 23 Agosti 2016

MUOGELEAJI WA MAREKANI ALIYEDANGANYA AKIMBIWA NA WADHAMINI


Wadhamini wanne wamemtosa muogeleaji wa Marekani mzushi, Ryan Lochte, wakiwemo watengenezaji wa Speedo na kampuni ya mavazi ya Ralph Lauren.

Uamuzi huo umekuja baada ya kampuni ya bidhaa za ngozi ya Syneron-Candela na ya Japan ya kutengeneza magodoro ya Airweave nao kujitoa kumdhamini Lochte.

Hatua hiyo ya wadhamini kumtosa Lochte inafuatia kitendo chake cha kudanganya kuwa ameibiwa kwa mtutu wa bunduki na polisi usiku akiwa Rio wakati wa Olimpiki.

Lochte, ambaye ameshinda mara 12 medali za dhahabu za michuano ya Olimpiki amekuwa akichuma mamilioni ya dola kutoka kwa wadhamini.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni