.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 29 Agosti 2016

RAIS MALINZI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA MUNISHI

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Kipa wa Young Africans na timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Deogratius Munishi kutokana na kifo cha Baba yake mzazi, Mzee Boniventur Munishi kilichotokea jana Agosti 28, 2016.

Rais Malinzi amepokea taarifa za kifo cha Mzee Boniventur Munishi mara baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) Young Africans na African Lyon uliofanyika jana Agosti 28, 2016 ambako Deogratius aliongoza timu yake Young Africans kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 bila kufahamu kuwa amepoteza baba.

“Ni ujasiri wa aina yake aliokuwa nao Kipa Munishi kwenye mchezo wa Ligi Kuu bila kuonyesha tofauti,” amesema Malinzi ambaye katika zake za rambirambi kwenda kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki amewataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa mpendwa wao.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Mzee Boniventur Munishi mahala pema peponi.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni