Goli
la dakika za mwisho la Leroy Fer limeipatia Swansea ushindi dhidi ya
Burnley katika moja ya michezo ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Uingereza
kwa msimu huu.
Golikipa
wa Burnley, Tom Heaton alishindwa kuudaka mpira wa krosi uliopigwa na
Jefferson Montero ambao ulimkuta Fer aliyeutumbukiza golini.
Leroy Fer akipachika wavuni goli pekee katika mchezo huo na kuipatia Swansea ushindi
Katika
mchezo mwingine goli la mpira wa kichwa lililofungwa na Solomon
Rondon lilitosha kuipatia West Brom ushindi mwembamba dhidi ya
Crystal Palace katika dimba la Selhurst Park.
Solomon Rondon akiwa juu hewani na kupiga mpira wa kichwa uliojaa wavuni na kuipa ushindi West Brom




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni