.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 14 Agosti 2016

ZLATAN IBRAHIMOVIC AJITAMBULISHA KWA GOLI WAKATI MAN UTD IKISHINDA

Zlatan Ibrahimovic amefunga goli katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya Uingereza wakati Manchester United ikiibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Bournemouth na kumpatia kocha wao mpya Jose Morinho ushindi wa kwanza.

Katika mchezo huo Juan Mata alikuwa wa kwanza kuifungia Manchester United katika dakika ya 40 kufuatia makosa yaliyofanywa na mabeki wa Bournemouth, ambapo baadaye katika dakika ya 59 Wayne Rooney alifunga la pili kwa mpira wa kichwa.

Zlatan Ibrahimovic alijitambulisha rasmi katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kufunga goli la tatu kwa shuti la mbali mnamo dakika 64 lililomshinda golikipa, kisha Adam Smith akaifungi Bournemouth goli pekee katika dakika ya 69.
    Juan Mata akifunga goli la kwanza la Manchester United baada ya mabeki kufanya uzembe
   Zlatan Ibrahimovic akiangalia shuti lake aliloachia likielekea wavuni na kuandika goli la tatu
   Mchezaji mpya wa Manchester United Eric Bailly akituliza mpira gambani huku akiwa ameruka juu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni