Zlatan
Ibrahimovic amefunga goli katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya
Uingereza wakati Manchester United ikiibuka na ushindi wa magoli 3-1
dhidi ya Bournemouth na kumpatia kocha wao mpya Jose Morinho ushindi
wa kwanza.
Katika
mchezo huo Juan Mata alikuwa wa kwanza kuifungia Manchester United
katika dakika ya 40 kufuatia makosa yaliyofanywa na mabeki wa
Bournemouth, ambapo baadaye katika dakika ya 59 Wayne Rooney alifunga
la pili kwa mpira wa kichwa.
Juan Mata akifunga goli la kwanza la Manchester United baada ya mabeki kufanya uzembe
Zlatan Ibrahimovic akiangalia shuti lake aliloachia likielekea wavuni na kuandika goli la tatu
Mchezaji mpya wa Manchester United Eric Bailly akituliza mpira gambani huku akiwa ameruka juu
Mchezaji mpya wa Manchester United Eric Bailly akituliza mpira gambani huku akiwa ameruka juu




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni