Mfalme Abdullah wa Saudi Arabia
Mahakama nchini Saudi Arabia
imeagiza mwanaume mmoja kuchapwa viboko 2,000 na kifungo cha miaka 10
jela, kwa kudharau Kuraan na kutoamini kama Mungu yupo akitumia
twitta yake.
Mwanaume huyo mwenye miaka 28,
amehukumiwa katika taifa hilo la Kiislam, baada ya polisi kubaini
kuwa katuma twitti 600 zenye kuonyesha imani yake ya kuwa hakuna
Mungu.
Chini ya Sheria za Saudi Arabia
zilizoanza kutumika miaka miwili iliyopita kutokuamini uwepo wa Mungu
ni sawa na kosa la kigaidi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni