Kocha wa Uingereza Sam Allardyce
amesema si jukumu lake kusema Wayne Rooney acheze nafasi gani, kauli
aliyoitoa wakati akipata ushindi wa kwanza wa goli 1-0 dhidi ya
Slovakia katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe.
Katika mchezo huo Uingereza ilipata
tabu kupata ushindi dhidi ya Slovakia iliyobakia na wachezaji 10,
kabla ya Adam Lallana kuipatia ushindi wa sekunde chache kabla ya
kipenga cha kumaliza mchezo.
Katika mchezo huo Rooney amefikisha
michezo 116 kushinda akiwa ni kapteni wa Uingereza, ambapo kwa jana
alijikita zaidi katika kucheza nafasi ya kiungo.
Kapteni Wayne Rooney akiwa kibaruani
Mpira uliopigwa na Adam Lallana ukitinga wavuni na kuandika goli pekee
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni