Luis Nani ameng'ara wakati Cristiano
Ronaldo akikosekana kwa kuifungia Ureno magoli mawili katika ushindi
wa magoli 5-0 dhidi ya taifa changa kisoka la Gibraltar, ukiwa ni
mchezo wa kwanza kwa mabingwa hao wa Ulaya.
Mchezo huo wa kirafiki uliofanyika
Porto, ulikuwa pia ni wa kwanza kwa Gibraltar tangu kupata uanachama
kutoka kwa shirikisho la soka duniani FIFA Mei mwaka huu, kuelekea
kufuzu michuano ya kombe la dunia 2018.
Luis Nani akiruka sarakasi baada ya kufunga goli
Kipa wa Gibraltar akiwa amekaa chini akimuangalia Nani
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni