Marekani imesema inaishutumu Urusi
kwa kuhusika na tukio la kushambulia msafara wa misaada karibu na mji
wa nchini Syria wa Aleppo siku ya jumatatu.
Maafisa wa Marekani wameviambia
vyombo vya habari vya nje, kuwa ndege mbili za Urusi zilihusika na
shambulizi hilo la msafara wa malori ya misaada.
Urusi imekanusha vikali kuhusika na
tukio yenyewe ama ndege za Syria na kusema tukio hilo limetokana na
moto ulitokea aridhini na wala si angani.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni