Tembo dume anayetumiwa kubeba
watalii na mizigo yao katika maporomoko ya maji maarufu nchini Cambodia
amemuua mmiliki wake kwa kumkangaya na kisha kuamua kukimbilia porini
kufuata tembo jike.
Mmiliki huyo Pop Sreang, 55,
aliuwawa akijaribu kumtuliza tembo huyo ili awabebe watalii na
alipogoma alimpiga na nondo kichwani ndipo alipopata tembo alipopandwa na hasira na
kumrusha juu na kisha kumkanyaga kanyaga.
Tembo akikatiza kwenye maji ya maporomoko hayo akiwa amembeba mtalii huku akiongozwa na mmiliki wake
Maporomoko hayo ya maji ya Cambodia ambayo ni maarufu kwa kuvutia watalii
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni