.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 9 Septemba 2016

WATALII WAKWAMA KWENYE MAGARI YA JUU YA MLIMA NA KULALA USIKU MMOJA

Makumi ya watalii wamekwama juu ya magari ya kutumia waya katika Mlima wa Alps nchini Ufaransa na kulazimu 45 kulala kwenye magari hayo usiku kucha, baada ya upepo mkali kusababisha hitilafu ya kiufundi.

Zoezi la uokoaji lilifanywa kwa watalii hao zaidi ya 110 kwenye magari hayo ya kukatiza juu ya mlima kwa kutumia kamba wakiwa juu umbali wa mita 50 katika eneo la Mont Blanc katika Mlima wa Alps.

Waokoaji wa mataifa ya Ufaransa, Italia na Uswizi jana usiku walitumia helkopta kuokoa watalii 65 kati ya 110 waliokuwa wamekwama, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Chamonix, Bernard Cazeneuve amesema. 
                      Waokoaji wakiwa wanafanya kazi ya uokoaji kwa kutumia helkopta
                                                Baadhi ya watalii waliookolewa wakiwa na furaha 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni