.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 8 Oktoba 2016

ASKOFU TUTU ABAINISHA UWEZEKANO WA KUOMBA KUSAIDIWA KUFA

Askofu Dedmond Tutu wa Afrika Kusini amebainisha kuwa anataka kuwa na fursa ya kuomba kusaidiwa kufa.

Mshindi huyo wa tuzo ya Nobel na mwanaharakati wa kupinga ubaguzi, amesema hataki kulazimishwa kuendelea kuishi kwa gharama zozote.

Matamshi hayo ya Tutu yameandikwa na yeye katika gazeti la Washghton Post wakati akitimiza miaka 85 ya kuzaliwa.

Mnamo mwaka 2014 Askofu Tutu alibainisha kuwa anaunga mkono wagonjwa mahututi kusaidiwa kufa, lakini alikuwa hajaeleza iwapo yeye pia angependa kusaidiwa kufa.

Mwezi uliopita Askofu Tutu alikuwa amelazwa na kufanyiwa upasuaji ili kumtibu maambukizi ambayo yamekuwa yakijirudia rudia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni