.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 22 Oktoba 2016

MIDDLESBROUGH YAGANGAMALA NA KUTOA SARE NA ARSENAL EMIRATES

Timu ya Arsenal imelazimika kutoka sare tasa na Middlesbrough ikiwa katika dimba lake la nyumbani la Emirates.

Baada ya kuisambaratisha Ludogorets Razgrad kwa magoli 6-0 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, Arsenal ilijikuta ikikabilina na upinzani mkali hii leo licha ya kumiliki mno mpira.

Middlesbrough inayonolewa na Aitor Karanka iliendelea kuonyesha upinzani mkali na kuifanya iambulie pointi moja, dhidi ya Arsenal iliyokuwa imeshinda michezo sita mfululizo.
 Kipa wa Arsenal Petr Cech alikuwa na kazi ya kuokoa michomo hatari ya Middlesbrough
Alexis Sanchez alishindwa kuzuia hisia zake za kuchanganyikiwa baada ya kukosa nafasi ya kufunga

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni