.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 27 Novemba 2016

CHELSEA YAREJEA KILELENI MWA LIGI KUU YA UINGEREZA

Chelsea imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza ikitokea nyuma baada ya kufungwa goli katika dimba la Stamford Bridge, na kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Tottenham.

Katika mchezo huo Tottenham walionekana wakiwa vyema baada ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kati kati ya wiki, na walikuwa wa kwanza kupachika goli kupitia kwa Christian Eriksen.

Tottenham inayonolewa na Mauricio Pochettino ilitawala kabisa mchezo huo hadi pale katika dakika za mwisho za kipindi cha kwanza, Pedro aliposawazisha goli kwa mpira wa shuti la kuzungusha uliojaa wavuni ukipitia katika kona ya juu ya goli.

Chelsea iliendelea kupambana kiume na alikuwa Victor Moses aliyefunga goli la pili, na kutibua rekodi ya Tottenhma ya kutokufungwa katika Ligi Kuu ya Uingereza kwa msimu huu. Pia amtokeo hayo yanaweka rekodi ya Tottehma kutoifunga Chelsea nyumbani kwa michezo 30.
Cristian Eriksen akifunga goli la kwanza katika mchezo huo huku mabeki wawili wa Chelsea wakiwa chini
              Pedro akijipinda kuachia shuti kali lililoenda kujaa wavuni na kuandika goli 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni