.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 27 Novemba 2016

CRISTIANO RONALDO HAKAMATIKI LA LIGA KWA KUFUNGA MAGOLI

Cristiano Ronaldo ameiongoza Real Madrid kupata ushindi dhidi ya Sporting Gijon katika dimba la Bernabeu, baada ya kufunga magoli mawili yaliyomfanya kuongoza kwa kufunga magoli mengi katika ligi ya La Liga.

Ronaldo amekuwa wa kwanza kufikisha magoli 10 katika msimu huu katika ligi hiyo, na kwa magoli mawili ya jana yalitosha kuinyima ushindi Sporting katika mchezo huo uliochezwa huku mvua ikinyesha.

Kwa ushindi huo wa magoli 2-1 umeifanya Real Madrid kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi saba dhidi ya timu ya Barcelona ambayo inashuka dimbani leo kucheza ugenini na Real Sociedad.
Kinara wa magoli La liga Cristiano Ronaldo akiachia shuti lililojaa wavuni na kuandika goli
Kocha Zinedine Zidane akiwa anatoa maelezo kwa wachezaji wake bila ya kujali mvua inayomnyeshea 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni