.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 27 Novemba 2016

SERGIO AGUERO AIOKOA MANCHESTER CITY NA KUIPA USHINDI

Sergio Aguero ametikisa nyavu mara mbili wakati Manchester City ikitokea nyuma baada ya kufungwa goli moja na kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Burnley katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Wenyeji Burnley walikuwa wapate penati, kabla ya kupata goli la kuongoza baada ya beki wa Manchester City Nicolas Otamendi kuokoa mpira vibaya na kumfikia kiungo Dean Marney aliyeachia shuti la yadi 25 na kujaa wavuni.

Manchester City walihangaika kurejesha goli hilo na alikuwa Sergio Aguero aliyeudokoa wavuni mpira baada ya mpira wa kona kumfikia. Goli hilo liliamsha ari kwa City ambapo krosi ya Fernandinho ilimkuta Aguero na kufunga goli la pili.
         Dean Marney akiwa ameachia shuti lililojaa wavuni na kuiandikia Burnley goli
     Sergio Aguero akishangilia na mchezaji mwenzake baada ya kufunga goli la ushindi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni