.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Novemba 2016

CRISTIANO RONALDO AFUNGA HAT-TRICK NA KUIZAMISHA ATLETICO MADRID

Cristiano Ronaldo amefunga hat-trick yake ya 39 katika maisha yake ya soka, na kuiongoza Real Madrid kuwafunga wapinzani wao wa jadi Atletico Madrid magoli 3-0 na kujikita kileleni mwa ligi ya La Liga.

Mshambuliaji huyo Mreno alifungua mvua ya magoli kwa kufunga kwa shuti la mpira wa adhabu lililogongwa na kumpoteza mahesabu golikipa wa Atletico Madrid Jan Oblak.

Ronaldo tena akaongeza la pili kwa mkwaju wa penati na kisha baadaye akatikisa goli la tatu akitumbukiza kimiani krosi ya Gareth Bale.

Real Madrid sasa wanaongoza La Liga kwa tofauti ya pointi nne, dhidi ya anayemfuatia Barcelona, ambao walidhibitiwa na kutoka sare taza na Malaga katika mchezo wa mapema jana.
                       Cristiano Ronaldo akifunga goli la kwanza kwa shuti la mpira wa adhabu
Cristiano Ronaldo akishangilia goli lake la tatu huku kipa wa Atletico Madrid akiwa kakaa chini mpira ukiwa wavuni

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni