.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 12 Novemba 2016

MASHABIKI WA POLAND WASABABISHA LEWANDOSKI KUPATIWA MATIBABU

Mshambuliaji wa Poland Robert Lewandoski anahitaji kufanyiwa matibabu baada ya flea (Flare) zilizorushwa na mashabiki wa timu yake kulipuka karibu yake katika mchezo mkali wa kuwania kufuzu kombe la dunia dhidi ya Romania.

Mshambuliaji huyo wa Beyern Munich hakujeruhiwa lakini alionekana kupatwa na mshtuko na hofu kwa tukio hilo lililotokea katika kipindi cha pili na kusababisha mechi hiyo kusimamishwa kwa dakika tano.

Katika mchezo huo ambao Poland waliibuka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Romania Kamil Grosiki alifunga goli la jitihada binafsi dakika ya 11, huku Lewandoski akifunga la pili katika dakika ya 82 na la tatu kwa mkwaju wa penati dakika ya 90.
   Robert Lewandoski akinyanyua mikono juu kulalamikia moto wa flea iliyorushwa karibu yake
                  Robert Lewandoski akiziba masikio baada ya flea iliyorushwa kulipuka
Robert Lewandoski akiwa anapatiwa matibabu huku akiziba masikio yake baada ya mlipuko wa flea

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni