.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 12 Novemba 2016

PAUL POGBA NA DIMITRI PAYET WAIPATIA USHINDI UFARANSA

Wachezaji Paul Pogba na Dimitri Payet wamecheka na nyavu wakati Ufaransa ikiathimisha mwaka mmoja wa mashambulizi la Paris kwa ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Sweden, katika mchezo wa kuwania kufuzu kombe la dunia.

Kabla ya kuanza mchezo huo uwanja mzima ulikaa kimya kwa dakika moja kuwakumbuka watu 130 wahanga wa mashambulizi hayo yaliyotokea Jijini Paris Novemba 13, 2015. Emil Forsberg aliifanya Sweden iongoze katika kipindi cha pili kwa goli la mpira wa adhabu.

Hata hivyo mchezaji wa Manchester United Paul Pogba alisawazisha haraka goli hilo na kisha baadaye Ufaransa ilipata goli la pili kupitia kwa Dimitri Payet katika dakika ya 65 na kuifanya iongozi kwa tofauti ya pointi tatu katika kundi lao.
                  Paul Pogba akiuangalia mpira alioupiga kwa kichwa ukielekea kutinga wavuni
        Dimitri Payet akipiga mpira ulioenda kujaa wavuni na kuiandikia Ufaransa goli la pili

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni