.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 3 Januari 2017

PENATI MBILI ZA JERMAIN DEFOE ZAINYIMA USHINDI LIVERPOOL

Jermain Defoe amefunga penati mbili wakati Sunderland ikitokea nyuma mara mbili na kupata pointi katika mchezo dhidi ya Liverpool iliyokatika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza

Liverpool ilipata goli la kuongoza kupitia kwa Daniel Sturridge kwa kichwa cha kubetua baada ya kuzembea kwa Dejan Lovren. Sunderland walisawazisha dakika sita baadaye kupitia kwa penati iliyopigwa na Defoe.

Sadio Mane aliwafungia wageni Liverpool goli la pili kwa shuti la kumalizia la karibu, lakini baadaye Mane akashika mpira na Defoe tena bila ajizi akatumbukiza mpira wavuni kwa mkwaju wa penati.
                                    Daniel Sturridge akiwa ameubetua kwa kichwa mpira uliojaa wavuni
                Jermain Defoe akiwa amejipinda kuachia shuti la mkwaju wa penati na kufunga

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni