Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na kuwaaga Mabalozi Sita wa
Tanzania walioteuliwa hivi karibuni kuwakilisha Taifa Nchini Mbali
mbali Duniani Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Balozi wa Tanzania Nchini Jamuhuri
ya Kidemokrasia ya Congo {DRC} Balozi Paul Mella kwa niaba ya wenzake
akimuahidi Balozi Seif kwenda kutekeleza majukumu yao kwa bidii za
kizalendo.
Balozi Seif akiwa katika picha ya
pamoja na Mabalozi wa Tanzania nchi za Nje mara baada ya kuzungumza
nao na kuwaaga rasmi kwenda kutekjeleza jukumu lao la Kidiplomasia,
kushoto ya Balozi Seif ni Balozi wa Tanzania Nchini Uswiss Dr. James
Nsekela na kulia yake ni Balozi wa Tnaznia Nchini Uturuki Balozi
Elizabeth Kiondo. (Picha zote na OMPR – ZNZ).
Press Release:-
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi alisema suala la kusimamia uhusiano wa
Kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Mataifa Rafiki Duniani ndio
kazi ya msingi kwa Mabalozi wote katika kutekeleza majukumu yao ya
kila siku.
Alisema Kazi ya Ubalozi inahitaji
uadilifu na ueledi mkubwa unaohitaji kuzingatia zaidi heshima na
Matakwa ya Taifa yatakayopelekea kuimarika kwa huhusiano uliotukuka
wa pande zote husika.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa angalizo
hilo wakati akiwaaga Mabalozi Sita walioteuliwa hivi karibuni na
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
kuiwakilisha Tanzania katika Mataifa mbali mbali Duniani.
Alisema Serikali ya Awamu
zilizopita nyuma iliwahi kulazimika kuwajeresha nyumbani na wengine
kuwafukuza kazi baaadhi ya Mabalozi wa Tanzania baada ya kushindwa
kuuheshimu Utumishi wao wa Kidiplomasia.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
alielezea matarajio yake ya mafanikio kwa kazi kubwa iliyofanywa na
Rais wa Jamuhuri ya MKuungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wa
kufanya upembuzi wa kina uliyoibuwa Watumishi hao wa Kidiplomasia
watakaokuwa kioo chema cha Tanzania katika Mataifa waliyopangiwa
kufanya kazi.
Akigusia suala la Maendeleo ya
Uchumi Zanzibar Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi aliwataka
Balozi hao wanaoiwakilisha Tanzania katika Mataifa mbali mbali
Duniani kuvitangaza Visiwa vya Zanzibar ambavyo kwa kiasi kikubwa
vitaendelea kuzitegemea Ofisi za Mabalozi hao.
Balozi Seif alisema Zanzibar hivi
sasa inategemea kupata zaidi mapato yake kupitia sekta ya Utalii
inayopata msukumo kutoka kwa Taasisi na Makampuni mengi ya nje hasa
Taifa ya Italy.
Alimuomba Balozi wa Tanzania Nchini
Ufaransa Balozi Samuel Shelukindo kuandaa mazingira ya kukutana na
Uongozi wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni {
UNESCO } lenye Makao Makuu yake Nchini humo kujadili na Wataalamu
wake kuangalia mazingira ya kuyahami Majengo ya Mji Mkongwe wa
Zanzibar ambao kwa kipindi kirefu uko chini ya hifadhi ya Urithi wa
Dunia.
Balozi Seif alisema majengo mengi
ndani ya Mji Mkongwe hivi sasa hayako katika mazingira mazuri jambo
ambalo Unesco ina wajibu wa kusaidia sambamba na kutoa ushauri badala
ya kuwa wakali katika kuelekeza pekee.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
aliwaeleza Mabalozi hao wa Tanzania Nchi mbali mbali Duniani kwamba
maeneo mengi ya Kihistoria yaliyopo katika Visiwa vya Zanzibar
ukiwemo Mji Mkongwe ni chem Chem ya kuimarika kwa mapato yake
kupitia sekta ya Utalii.
Balozi Seif Ali Iddi alimuagiza
Balozi wa Tanzania Nchini Uturuki Balozi Elizabeth Kiondo kufuatilia
mahusiano na Mikataba iliyopo ya muda mrefu kati Uturuki na Tanzania
na Zanzibar kwa Ujumla.
Alisema ipo mikataba mingi
iliyokwishatiwa saini kati ya Uturuki na Zanzibar katika sekta mbali
mbali ikiwemo ile kubwa ya Utalii ambayo inastahiki kufuatiliwa
muelekeo na utekelezaji wake.
Naye kwa niaba ya Mabalozi hao wa
Tanzania Nchi mbali mbali Ulimwenguni, Balozi wa Paul Mella
anayekwenda nchini Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo { DRC }
alimuahidi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba watazingatia
jukumu walilopewa na Taifa katika kutekeleza wajibu wao.
Balozi Paul alisema Watanzania wana
haki ya kujenga matumaini makubwa kutoka kwa Kikosi hicho mahiri
kinachoelekea katika eneo lake la uwajibikaji kuisimamia na
kuitangaza Diplomasia ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar
11/2/2017.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni