.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 11 Februari 2017

RAIS DONALD TRUMP APANGA KUTOA AGIZO JIPYA LA KUZUIA WANAOINGIA MAREKANI

Rais Donald Trump anapanga kutoa agizo lake jipya la kuwapiga marufuku raia wa baadhi ya mataifa kuingia Marekani, baada ya jaribio lake la awali kuzuiliwa na mahakama.

Bw. Trump amewaambia waandishi wa habari akiwa kwenye ndege ya rais Air Force One, kwamba agizo hilo jipya atalitoa mapema jumatatu ama jumanne.

Uamuzi huo wa Trump umekuja baada ya mahakama ya rufaa ya San Francisco kukazia uamuzi wa mahakama ya chini kuzuia agizo lake.

Agizo la rais Trump lililenga kupiga marufuku kuingia Marekani raia wa mataifa saba ya Kiislam.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni