.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 29 Machi 2017

TEKNOLOJIA YA VIDEO YATUMIKA KUAMUA MCHEZO WA HISPANIA NA UFARANSA

Teknolojia ya video imetumika kurekebisha maamuzi ya makosa ya waamuzi katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki ambao Hispania iliifunga Ufaransa magoli 2-0 Jijini Paris.

Mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann goli lake lilikataliwa kwa msaada wa teknolojia ya video kutokana na kuotea.

Goli la pili la Hispania lililofungwa na Gerard Deulofeu, lilikubaliwa na teknolojia ya video baada ya mshika kibendera kuashiria kimakosa kuwa ameotea.

David Silva aliifungia Hispania goli la kwanza kwa mkwaju wa penati baada ya Laurent Koscielny kumchezea rafu Deulofeu.
Gerard Deulofeu akifunga goli lililokataliwa na mshika kibendera lakini likakubaliwa na teknolojia ya video 
                   Mtaalam wa teknolojia ya video akiufuatilia mchezo huo kwa umakini

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni