.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 27 Aprili 2017

RAIS DK.MAGUFULI KUPOKEA TAAARIFA YA ZOEZI LA UHAKIKI WA VYETI KWA WATUMISHI WA UMMA



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz

Faksi: 255-22-2113425



OFISI YA RAIS,
      IKULU,
 1 BARABARA YA BARACK OBAMA,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ikulu, Chamwino,Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kesho tarehe 28 Aprili 2017, atapokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti kwa Watumishi wa Umma katika Ukumbi wa Chimwaga Mkoani Dodoma.

Taarifa hiyo itawasilishwa kwa Mheshimiwa Rais na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mheshimiwa Angellah Kairuki.

Zoezi la uhakiki wa vyeti kwa Watumishi wa Umma liliendeshwa na Serikali kuanzia Mwezi Oktoba mwaka 2016.

Jaffar Haniu,
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU,
Chamwino, Dodoma.
27 Aprili, 2017

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni