.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 1 Aprili 2017

ROGER FEDERER AMFUATA RAFAEL NADAL FAINALI MICHUANO YA MIAMI OPEN

Roger Federer ameshinda mchezo mkali uliodumu kwa muda wa saa tatu dhidi ya Nick Kyrgios na kupata nafasi ya kutinga fainali dhidi ya Rafael Nadal katika michuano ya tenesi ya Wazi ya Miami.

Mchezaji huyo raia wa Uswizi ameshinda mchezo huo kwa seti 7-6 (11-9) 6-7 (9-11) 7-6 (7-5) na kufanya rekodi yake ya mwaka 2017 kufikia ushindi wa michezo 18 bila ya kupoteza hata mmoja.

Federer atamvaa Nadal kwa mara ya 37 siku ya jumapili, na mara ya pili kwa mwaka huu baada ya kumfunga Mhispania huyo mwezi Januari katika michuano ya tenesi ya Wazi ya Australia.
                    Roger Federer akipeana mkono na Nick Kyrgios baada ya kumshinda
                 Roger Federer akishangilia kwa kuiangalia kamera baada ya kushinda 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni