Uhamisho wa Paul Pogba, ulioweka
rekodi dunia kutoka Juventus kuja Manchester United mwaka jana
unafanyiwa uchunguzi na Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA).
Shirikisho la Soka Duniani
limeiandika klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza kutaka ufafanuzi juu
ya makubaliano yalivyofikiwa.
Fifa inatilia shaka namna kitita cha
paundi milioni 89.3 cha uhamisho wa Pogba, kilivyogawanywa kwa
wahusika.
Hii ni baada ya kubainishwa na
Sportsmail, kuwa wakala wake Mino Raiola alipata paundi milioni 41.
Wakala wa Paul Pogba Mino Raiola


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni