.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 1 Mei 2017

RAIS ZUMA AONDOKA KWA HASIRA KWENYE MKUTANO WA MEI MOSI BAADA YA KUZOMEWA

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ameondoka katika mkutano wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) baada ya kuzomewa na wafanyakazi wakishinikiza ajiuzulu urais.

Ngumi pia zimetokea katika mkutano huo baina ya wafuasi wanaomuunga mkono rais Zuma na wapinzani wake jambo lililopelekea hotuba zote zilizopangwa kutolewa kwa ajili ya Mei Mosi kutotolewa.

Shirikisho la Wafanyakazi nchini humo COSATU, lilitoa wito mwezi uliopita wa kumtaka rais Jacob Zuma kuachia madaraka baada ya kumfukuza kazi waziri wa fedha anayekubalika mno.

Licha ya kuwepo kwa shinikizo la kumtaka kujiuzulu rais Zuma ameapa kubakia madarakani hadi hapo muhula wake utakapomalizika mwaka 2019.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni