Dani Alves amefunga goli katika
mchezo wake wa kwanza wakati Paris St Germain ikiwafunga mabingwa wa
Ligi 1 Monaco kwa magoli 2-1 na kutwaa kombe la mabingwa.
Katika mchezo huo Djibril Sidibe
alikuwa wa kwanza kuziona nyavu na kuifanya Monaco kuongoza baada ya
kuubetua mpira na kumshinda kipa Alphonse Areola.
Lakini Alves, aliyenunuliwa akitokea
Juventus kwa uhamisho huru mapema mwezi huu alifunga goli la
kusawazisha katika dakika ya 51.
Alves tena alimpikia goli Adrien
Rabiot aliyeifungia Paris St Germain goli la pili na kuibuka mabingwa
kombe hilo linalojulikana Kifaransa kama Coupe de France.
Dani Alves akiachia shuti na kufunga goli akiichezea kwa mara ya kwanza PSG
Dani Alves akibusu kombea la washindi la Coupe de France baada ya kukabidhiwa
Wachezaji wa Paris St Germain wakishangilia baada ya kukabidhiwa kombe
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni