Gari linalomilikiwa na chama cha
muungano wa Jubilee cha Rais Uhuru Kenyatta limetekwa katika eneo la
Mandera na wapiganaji wanaohisiwa kuwa ni wa kundi la Al-Shabaab.
Mkuu wa Polisi wa Mandera Kusini,
Charles Chacha, amesema tukio hilo limeripotiwa jana majira ya saa 11
jioni, ambapo dereva na abiria nao hawajulikani walipo.
Amesema gari hilo limetekwa katika
mji wa Bore Hole 11 baada ya kuwashusha wafuasi wa Jubilee eneo la
Falama karibu na mpaka wa Kenya na Somalia.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni