Jukwaa la WAA (Women Advancing
Africa) - limejipanga kukutanisha wataalamu na nguli wa Afrika
kutatua changamoto muhimu kwa pamoja na kutengeneza agenda ya
kuendesha maendeleo ya kiuchumi ya wanawake Afrika
Tarehe 27 Julai 2017, Dar es Salaam
- Maandalizi ya mwisho ya ufunguzi wa Jukwaa la Women Advancing
Africa (WAA) yanaendeleayakiwa ni jitihada za Pan Afrika mpya
zilizoanzishwa na Graça Machel Trust kutambua na kusherehekea nafasi
na ngazi muhimu ambayo wanawake wanaishikilia katika kuleta maendeleo
ya Afrika na kuendesha mageuzi ya kijamii na kiuchumi.
Kongamano
litafanyika kuanzia Agusti 9 hadi 12 jijini Dar es Salaam, Tanzania
katika hotel ya Hyatt Kilimanjaro.
Akizungumzia kuhusu kwanini taasisi
hiyo imeanzisha jukwaa la WAA, Mama Graça Machel amesema “Japo
kuwa Afrika imeshuhudia maendeleo makubwa sana katika miongo ya hivi
karibuni, pengo kubwa katika maendeleo ya wanawake kiuchumi linabakia
kuwa changamoto.
Tuko katika zama zingine za ukombozi
– ukombozi wa wanawake kiuchumi. Wanawake hawawezi kutengwa tena na
kwa kupitia Women Advancing Africa, Taasisi inataka kuwawezesha
wanawake kuchukua nafasi ya muhimu katika kuendeleza uchumi wa
Afrika. Taasisi inatoa jukwaa la wanawake kudai haki yao ya kukaa
katika meza ambako maamuzi yanafanyika na kubadilisha sera, mipango
na mikakati kwa ajili ya baadae na kizazi kijacho”.
Taasisi imepata heshima ya kujiunga
kwa Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na
mjumbe wa Sekretariet kuu ya Umoja wa mataifa UN wa Jopo la Ngazi ya
juu katika Uwezeshaji kiuchumi wa Wanawake (Women’s Economic
Empowerment) Samia Sululu Hassan katika jukwaa la WAA, kwaajili ya
kutoa mtazamo wake katika masuala ambayo yatajadiliwa katika kipindi
cha siku nne cha kongamano hilo.
Kongamano litakuwa na vipindi vya
mahojiano ambavyo vimeandaliwa katika misingi mikuu mitatu.
Ujumuishaji wa kiuchumi, Upataji wa masoko na Mabadiliko ya kijamii.
Mchangamano wa rika na mchangamano
wa kisekta wa washiriki katika Kongamano la WAA Kwa makadirio ya mahudhurio ya
washiriki 200 kutoka barani kote, kongamano la WAA litakusanya pamoja
mchanganyiko wa wanawake na vijana watakaowakilisha viongozi na
wahamasishaji kutoka katika sekta binafsi, taaluma,taasisi za umma,
serikali, taasisi za kimaendeleo na vyombo vya habari ambavyo
vitaleta sauti zao, uzoefu wao na mawazo yao kwaajili ya kuweka
mikakati, kuweka vipaumbele na kutengeneza agenda ya pamoja katika
kuendesha mageuzi ya kijamii na kimaendeleo ya Afrika.
Idadi kadhaa ya wazungumzaji katika
sekta muhimu kama vile migodi na uchimbaji, kilimo biashara, Benki,
mawasiliano, vyombo vya habari, huduma za afya, bidhaa na huduma
wataleta ujuzi na utaalamu wao katika kongamano.
Wazungumzaji
mashuhuri watakuwepo wakiwemo Leymah Gbowee mwanaharakati wa kutetea
amani wa Liberia na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel, Vera Songwe
Katibu mkuu wa Tume ya Uchumi ya Umoja Wa Mataifa, Dk. Monique
Nsanzabaganwa, Gavana Msaidizi wa Benki ya Taifa ya Rwanda, na
Sheila Khama, Meneja Mtendaji kwenye kitengo cha Benki ya Dunia cha
Sekta ya Madini cha Kimataifa.
Agenda ya Maendeleo ya Jamii
Kutakuwa na mfululizo wa matukio ya
pembeni yatakayofanyika sambamba na kongamano la WAA kuhusu masuala
mbalimbali ikijumuisha virutubisho na chakula bora, elimu na ndoa za
utotoni, uongozi na mazingira bora ya kazi, kuleta umuhimu wa
mabadiliko ya kijamii kama kipengele muhimu cha kutazama mwanamke kwa
ujumla wake n.k.
Kongamano la WAA pia litasherehekea
tamaduni anuai za Afrika na ubunifu katika mifumo yake yote, kuanzia
katika Lugha, mpaka katika ubunifu na mitindo, na utengenezaji wa
filamu na kucheza ngoma. Kongamano la mwaka huu litasherehekea
waandishi na wasimulia hadithi ambao wanatoa changamoto kwa waandishi
waliopo, wakiwa wanabadilisha usimuliaji na kutengeneza ujuzi wa kina
wakupongezw pamoja na sekta ya viwanda na jukumu lao katika
kuendeleza maendeleo ya kijamii.
Utafiti unaotazama katika masimulizi
na ushiriki wa wanawake katika uchumi Afrika.
Ripoti mbalimbali zitazinduliwa
wakati wa kongamano hilo. Pamoja na Tume ya Uchumi ya umoja wa
Mataifa kwa Afrika (United Nations Economic Commission for Africa
(UNECA), Graça Machel Trust itazindua uchunguzi kuhusu Uchumi wa
mwanamke wa Afrika “The Female Economy in Africa”.
Utafiti huo
utachambua ushiriki wa kazi za wanawake katika Afrika, wakijikita
katika uwiano wa kijinsia katika uchumi, ushiriki katika siasa za
taifa, ushiriki katika fedha na ubaguzi wa kisekta. Uchunguzi huo
utatoa msingi wa namna ya kupima na kufuatilia maendeleo katika
shughuli za wanawake wakiwa wanatoa hali halisi katika taarifa
zitakazo kuwa zinasambazwa.
Mtandao wa wanawake walioko katika
vyombo vya habari wa Graça Machel Trust pia utazindua ripoti ya
utafiti kuhusu uwasilishaji wa mwanamke katika vyombo vya habari
itakayokuwa inaitwa: women in media - Masimulizi ni yapi?” kipindi
hicho kitatangazwa kama kipindi cha moja kwa moja katika mtandao wa
Facebook, kutakuwa na ushiriki wa moja kwa moja kwaajili ya kuchochea
mazungumzo mapana zaidi kuhusu masimulizi ya mwanamke katika vyombo
vya habari pamoja na mifumo mingine ya usimuliaji.
Tangazo litatolewa
katika tovuti ya WAA www.WomenAdvancingAfrica.com na ukurasa wa
facebook wa WAA, www.Women Advancing Africa – WAA, muda wake
ukikaribia.
Kidokezo kingine katika uzinduzi wa
forum ya WAA itakuwa ni uzinduzi wa kitabu (coffee table book)
kinachosherehekea juhudi za wanawake katika biashara kikiwa na
mkusanyiko wa masimulizi ya kuhamasisha kutoka Botswana, Burundi,
Cameroon, Jamuhuri ya Demokrasia ya Congo, Ethiopia, Ghana, Kenya,
Malawi, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Rwanda, Senegali, Afrika Kusini,
Tanzania, Uganda, Zambia na Zimbabwe.
Wanawake watengenezao utajiri:
mkusanyiko wa masimulizi ya wanawake wajasiriamali kutoka Afrika
nzima. Kitabu hicho kitajumuisha idadi kubwa ya wanawake wanaofanya
ujasiriamali kutoka katika mtandano wa wanawake wa taasisi ya Graca
Machel Trust na kimewekewa utangulizi na Mama Machel.
Mwenendo wa wanawake waliojikita
katika kujiendeleza kiuchumi.
Akielezea nini kinaifanya WAA kuwa
ni jukwaa la kipekee, Mama Machel alihitimisha kwamba, “Uendelezaji
wa wanawake Afrika unatoa nafasi kuleta pamoja nguvu, uboreshaji na
ubunifu wa wanawake kutoka kila pembe ya Afrika kwaajili ya kutoa
suluhisho na kutufanya wote tuwe imara, tulioungana na tusioweza
kuzuilika.
Jukwaa hii kweli ni kichochezi katika kutengeneza vuguvugu
kubwa zaidi la wanawake waliojikita katika kuendeleza wanawake
kiuchumi ambao kwa pamoja wanaijenga na kuiendesha agenda ya
maendeleo ambayo itakuwa inapimika na endelevu”.
Kwa upana wa
mtandao wa Pan Afrika ambao unafikia nchi 20, Graça Machel Trust
itasaidia kupanua mtandao wa wanawake katika kilimo, biashara na
ujasiriamali, fedha na vyombo vya habari kwa kushirikiana na mtandao
mkubwa wa WAA kuchochea kongamano hilo kufanikisha utendaji ambao
unapimika na matokeo endelevu.
Kuwa sehemu ya jitihada hizi zenye
msisimko, unaweza kujiandikisha hapa au kushiriki moja ya maonyesho
yake au matukio ya ziada yaliyopo.
Taasisi ya Graca Machel Trust
inapenda kuwashukuru wadau wenye roho njema ambao wamewezesha
kufanikisha ndoto yao kuwa kweli. Shukurani za pekee ziende kwa UPS
Fondation, Intel Foundation, American Tower Corporation na UN Women.
Vyombo vya habari washirika ikiwemo: ABN360 Group, ikijumuisha CNBC
Africa na Forbes Africa; Nation Group na chombo cha habari cha hapa
Tanzania Azam Media Group. APCO Worldwide imefanya kazi kwa karibu
sana na taasisi ya Graça Machel Trust, katika kutoa ujuzi na
mwongozo kwenye kuunda mtandao huu wa kipekee wa wanawake. Washirika
hawa wanakubaliana na imani ya taasisi hii kwamba kumuendeleza
mwanamke kiuchumi ni muhimu kwaajili ya maendeleo endelevu ya familia
za kiafrika, jamii na taifa.
Imetolewa na:
Mkurugenzi wa mawasiliano wa Graça
Machel Trust: Rosemary Viljoen,
Barua Pepe:
RosemaryV@GracaMachelTrust.org
Namba za simu za Maneja Mahusiano wa
Vyombo vya Habari APCO: Anthony DeAngelo,
(t) +1.202.778.1000
(m) +1.202.702.7510
Barua pepe:
ADeAngelo@APCOworldwide.com
IJUMAA, JULAI 28, 2017
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni