.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 12 Agosti 2017

ARSENAL YAANZA LIGI KWA USHINDI, LACAZETTE AKIONESHA MAKALI YAKE

Mchezaji aliyetokea benchi Olivier Giroud amefunga goli zuri la ushindi wakati Arsenal wakipambana kutoka nyuma na kuifunga Leicester City magoli 4-3 katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu wa 2017-18.

Arsenal ilikuwa nyuma kwa magoli 3-2 zikiwa zimebakia dakika saba tu mpira kumalizika kabla ya Aaron Ramsey na Giroud kubadilisha matokeo ya mchezo huo na kuwafanya wenyeji kuibuka na ushindi katika dimba la Emirates.

Katika mchezo huo mchezaji mpya wa Arsenal Alexandre Lacazette alifunga goli la kwanza ndani ya sekunde 94 akishuka mara ya kwanza dimbani katika ligi hiyo lakini Shinji Okazaki akaisawazishia Leicester City dakika mbili baadaye.

Jamie Vardy aliongeza goli la pili lililotokana na krosi ya Marc Albrighton kabla ya Danny Welbeck kufunga goli la kusawazisha. Vardy tena akafunga goli akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Riyad Mahrez.
        Shinji Okazaki akiruga juu na kufunga kwa mpira wa kichwa katika mchezo huo
                                             Mshambuliaji Danny Welbeck akiifungia Arsenal goli
Kipa wa Leicester City, Schmeichel akijaribu bila mafanikio kuzuia mpira wa kichwa uliopigwa na Olivier Giroud 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni