Vita baridi inaonekana kufukuta kati
ya bodi ya klabu ya Barcelona na wachezaji kufuatia Lionel Messi
kuweka picha yake akiwa na Neymar, baada ya klabu hiyo kutangaza nia
ya kumshtaki nyota huyo wa PSG.
Inaonekana kuwa Lionel Messi sasa
amebainisha matatizo yaliyopo ndani ya klabu hiyo baada ya kuposti
kwenye Instagram yake picha yake hiyo aliyoipiga akiwa pamoja na na
Nemyar na Luis Suarez.
Timu ya Barcelona jana ilitangaza
kuwa itampeleka Mahakamani Neymar kwa kushindwa kuheshimu kifungu cha
kuongeza mkataba na klabu hiyo alichosaini katika mkataba wake
alioingia mwaka jana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni